chakarika

Wednesday 6 October 2010

Mficha uchi hazai

Mimi naitwa jina langu Sijali nimelelewa na nyanya wangu nikiwa mdogo na kwa babati nzuri nikasoma elimu chekechea katika kituo cha wazungu. Sasa raha na tabu ya umombo na mchanganyiko wa lugha za kigeni kutoka ulaya zilinisababisha kuwa na wakati mgumu sana pale gharama ya kusoma shule pamoja wazungu ilipokuwa kubwa kuliko uwezo wa kifedha kumudu gharama ya ada kutoka kwa nyanya wangu. Basi nikalazimika kujiunga na darasa la kwanza kwenye shule zetu za serikali.

Lugha rasmi katika shule za msingi hapa Tanzania kama inavyofahamika ni Kiswahili tangu darasa la kwanza mpaka kufikia darasa la saba. Ingawa kwa wakati huo lugha ya kiengereza ilitumika kama somo utakapofikia darasa tatu. Sasa hali ilikuwa ngumu kweli kwa upande wangu katika kusoma na kuandika lugha ya Kiswahili, ingawa kuongea haikuwa shida.

Somo la hisabati kwa sababu lenyewe sehemu kubwa ya shughuli zake za kiada zinategemea tarakimu na pia kama lugha moja duniani. Hivyo haikuwa na shala isipokuwa tuu. Iwapo swali kama linatakuwa limeandikwa ama kutungwa kwa maneno ya Kiswahili basi hali iliendelea kuwa mbaya.

Kimsingi nilikuwa sijishughulishi kabisa na hali hiyo maswali yanayokuwa na maelezo tena hasa ya Kiswahili, nikitegemea kwamba iwapo sitajibu basi yale maswali hisabati yenye tarakimu ambayo nilikuwa mzuri sana kwenye hilo yatanilinda kupata alama. Kitu cha kusikitisha masomo mengine yote yaliobaki yalikuwa na sifa(kusoma na kuandika,) ambazo mimi sikuwanazo.

Sasa kwa sababu za bora liende la mwalimu wetu wa darasa la kwanza, na wakati huo ilikuwa mwalimu anayeanza wanafunzi darasa la kwanza alikuwa akiendelea na wanafunzi kuingia darasa la pili. Hivyo mimi niliendela na ubovu wangu huo bila ya kupata usaidizi wa karibu wa kutoka mwalimu na mimi kama mwanafunzi nisiye fahamu kwamba hicho nachofanya kitaniletea madhara maishani.

Nikawa naona ni unafuu na ujanja kumtoroka mwalimu na kuishi kama mwanafunzi ambaye hawezi kusoma ama kuandika.Sasa hapo nyumbani nilipokuwa naishi ndipo palipoweza kugundulika udhaifu wangu maana huyo nyanya yeye kitaaluma alikuwa ni Mwalimu.

Siku moja akaniomba ripoti ya kimasomo yangu ya jumla ya mwaka ya darasa la pili wakati huo tulikuwa tunakabidhiwa wanafunzi na kuleta nyumbani . Mimi nilikuwa na ujanja wa kubadirisha tarakimu.

Hivyo nilijichanganya zile sehemu ambazo unatakiwa ujue kusoma na kuandika lugha kiswahili ili kuweza kurekebisha. Sasa sehemu inayojaza na nafasi ya mwanafunzi darasani kwenye tarakimu ilionyesha nipo nafasi ya kumi na nane kati ya wanafunzi mia moja, Ingawa ukweli wenyewe nilikuwa na nafasi ya tisini na nane.

Na hiyo ndiyo maneno yalikuwa yameandikwa kwa lguha ya Kiswahili. Basi nyanya yangu akashtukia kitu pale.Akasema naomba kachukue kile kitabu cha darasa kwanza cha Juma na Roza, Nategemea kila mtu aliyesoma wakti huo anakifahamu vizuri. Akafungua ukurasa mmoja nisome. Nilipoona tuu picha nikakumbuka ile hadithi niliyosomewa na baadhi marafiki zangu niliyokunasoma nao. Nikaaanza kusoma kwa jinsi nilivyokariri. Maana suala ilo nilikuwa mzuri na hodari sana wakukariri.

Nyanya yangu aukupata kitu hapo ingawa bado taaluma yake ilikuwa inamwambia kuwa kuna kitu kinaendelea upande, baada ya kuona mkorogo kwenye taarifa yangu ya mwaka ya kimasomo. Sasa tatizo kubwa ilikuwa wakati huo shule zimefunga hivyo hawezi kufuatilia mpaka ya mwezi na nitakuwa naingia darasa la tatu.

Kutokana na hali basi alihamua kunikabidhi kwa mwalimu mwenzake ambaye anasifikia kwa kufundisha vizuri na kufuatilia maendeleo ya mwanafunzi. Basi ya baada kufungua shule niliambiwa na Nyanya yangu kwamba nalazimika kukaa na huyo mwalimu kwenye darasa kwa muda wa juma moja kabla sijaendelea na darasa la tatu.

Kwa kuanzia tuu yule mwalimu alikuwa hatumii kitabu katika kusoma ama kuandika. Hivyo hadithi yeyote iliyopo kitabuni inaandikwa ubaoni tena bila picha. Sasa hapo na mimi nilikuwa nimepangiwa nikahe kiti cha kwanza kabisa, na pia nilichaguliwa kuwa mtu wa kwanza kusoma kwa siku hiyo, tena unatumia fimbo kuonesha maneno unayosoma, neon moja baada la jingine.

Na hapo ndiyo siri yangu ilipofichuka tena darasa lote wakijua kwamba siwezi kusoma na kuandika Kiswahili. Na pia hiyo taarifa ikawa imemfikia Nyanya wangu. Na hiyo ndiyo ilikuwa tiketi ya kubaki lile darasa la pili badala ya kuendelea darasa la tatu.

Nakubali na pia naamini yule mwalimu aliyetumia ujanja wa kujua siri yangu na nyanya wangu hawa wote walikuwa wananitakia mema maishani mwangu. Maana huyo mwalimua na huyo nyanya wote wamefariki hivi sasa wakati naandika hii habari kwa kifupi kuhusu maisha yangu huko nyuma.

Kimsingi nataka kuzungumzia siasa za hapa nyumabani Tanzania kwamba wananchi waache kuchagua viongozi kwa mazoea maana hayawezi kukusaidia kwa mikakati ya muda mrefu. Iwapo unahitaji maendeleo tusiendelee mpaka watokee malaika kama hawa walionisaidia mimi leo kuweza kujua kusoma, kuandika Kiswahili.

Kupiga kura kwa kiongozi kwa sababu mazoea utaishia kuwa kama mimi nilivyokuwa katika elimu ya awali mzuri wa tarakimu tuu na siyo maandishi anayepata hasara hapo ilikuwa ni mimi, Wakti mwalimu yeye alikuwa akiendelea kulipwa mshahara wake. pamoja kuwa nilikuwa sipati maarifa yoyote kutoka kwa yule mwalimu wa kwanza. Hivyo unapochagua viongozi wabovu pia inapelekea kuwa na maamuzi mabovu.

Siasa ni muhimili wa nchi kwa kila jambo, tusichagua wabunge, madiwani na hta pia rais kwa ajili ya mazoea. Iwapo kama tunataka na pia tunahitaji maendeleo basi hilo halina mjadala kiongozi anatakiwa awe shupavu wa utendaji anafuata misingi na sheria zilizopo na siyo maneno na ubabaishaji.

Ambayo kimsingi kama ni Rais, au mmbunge ataendelea kupokea mshahara na posho. Wakati huo huo sisi wapiga kura tukiendelea kuwa maisha shida na dhiki isiyokuwa na kipimo.

Inaendeleo siku zijazo hizi zitakuwa makala mfululizo kadri navyopata muda wa kuandika

No comments:

Post a Comment