chakarika

Tuesday 12 October 2010

Bado tumejifunga katika mantiki iliyopinda





Jenerali Ulimwengu Oktoba 6, 2010


SIKU zinazidi kuyoyoma, na uchaguzi uliosubiriwa na wengi unazidi kukaribia. Hamasa zinazidi kupamba moto na shauku za washiriki wa kila aina zinazidi kujidhihirisha.

Kama ilivyo kote katika bara letu, Afrika, uchaguzi unabeba umuhimu ambao haupatikani katika nchi za wenzetu walioendelea. Kwa wenzetu katika nchi zilizoendelea, kipindi cha uchaguzi ni kipindi cha kujipima nguvu kwa mara nyingine na kushindanisha sera na kuomba ridhaa ya wananchi wakubali kuongozwa na mmoja wa washindani.

Hakuna vita, hata kama wakati mwingine maneno yanakuwa makali na wanasiasa watabeza na kukejeli washindani wao. Ni mara chche sana itasikika kwamba wafuasi wa chama kimoja wamepigana na kutoana ngeu na wafuasi wa chama kingine, au kusikia kwamba jeshi la polisi limefyatua risasi na kuwajeruhi wafuasi wa cha fulani.

Mambo yanakuwa shwari, kampeni zinaendeshwa kwa amani, na kura zinapigwa katika utulivu, na ingawaje imewahi kutokea kukawa na ubishani kuhusu matokeo (kama baina ya Joji W. na Al Gore) si kawaida kusikia malalamiko kuhusu hilo.

Kimsingi hali hii inatokea katika nchi za wenzetu kwa sababu uchaguzi, ingawa ni muhimu, si suala la kufa na kupona. Watu hushiriki katika kampeni kwa nguvu zao zote, wakalumbana kwa hoja zilizopangiliwa vyema, wakacheza dansi, wakaimba, wakafanya matamasha kila mahali wakiburudika, kisha wakapiga kura. Wanaoshinda wanapongezana, na wanaoshindwa wanaliwazana. Kisha wote wanarejea katika shughuli zao za kawaida.

Hawa wana shughuli zao za kuwapa riziki, na ambazo ndizo muhimu kuliko uchaguzi ambao kwao ni zoezi la msimu. Wanarudi katika uzalishaji na utoaji huduma hadi kipindi kingine cha uchaguzi kitakapowadia.

Afrika ni tofauti kabisa. Kila uchaguzi unachukuliwa kama vita, ni suala la kufa na kupona. Tofauti na hali ya wenzetu niliowaeleza hapo juu, washiriki wengi katika michakato ya uchaguzi katika nchi za Afrika hawana shughuli yo yote nyingine ya kufanya. Hawamo katika uzalishaji wala utoaji huduma; hawana ajira.

Aidha, katika nchi takriban zote za Afrika, uchaguzi ndio unaamua ni akina nani ‘watakula’ kwa kipindi chote hadi uchaguzi mwingine utakapofanyika, na akina nani watanyimwa ‘mlo’ kwa kipindi chote hicho, kwa maana ya kwamba anayeshinda anashinda na kuchukua kila kitu na anayeshindwa anapoteza kila kitu, siyo yeye mwenyewe pekee bali pia ndugu, jamaa, marafiki na washirika wake wote.

Ushindi katika uchaguzi wa Kiafrika hufungua milango ya neema kubwa kwa mshindi na washirika wake. Kinara wa ushindi huo, ambaye mara nyingi huitwa ‘rais’, anakuwa ndiye kisima cha kila kitu: mamlaka ya dola; uwezo wa kumfanya ye yote asiye kitu kuwa mtu; uwezo wa kufikiri kuliko mtu ye yote mwingine; ukwasi na utajiri usiotokana na juhudi ya uzalishaji wala biashara; tunu ya kuwa na wanafamilia wanaojitokeza ghafla kuwa wenye akili na uwezo mkubwa, na kadhalika.

Yule anayeshindwa, hali yake ni mbaya sana, kwani kushinda si kupoteza uchaguzi tu na fursa ya kutoa mchango katika kuisaidia jamii kuendelea; ni zaidi ya hilo. Kwanza aliyeshindwa huonekana kama mkorofi, kwa sababu tu alithubutu kushindana na yule aliyeshinda.

Namna gani yule anayekuja kushindwa anaweza kujua nani atashinda tangu mwanzo ili asimpinge akaonekana mkorofi baada ya kuwa ameshindwa? Hili ni swali gumu, lakini mantiki ya siasa za Waafrika ni kwamba aliyeshindwa ndiye mkorofi, ndiye mwenye uchu wa madaraka, ndiye anayewagawa wananchi na ndiye mwenye kutaka kuleta vurugu nchini. Hiyo ndiyo mantiki iliyopinda ya Waafrika wengi walio madarakani.

Lakini ukorofi wa yule ambaye hatimaye atashindwa hudhihirika pale ambapo huyo mshindani mkorofi anapompinga aliye madarakani, ndiyo kusema yupo mtawala madarakani, na anaendesha serikali yake vizuri tu, naye anaamini kwamba kazi yake anaifanya kama anavyotakiwa, halafu anajitokeza mtu mwingine kusema anataka jukumu la kuongoza nchi akabidhiwe yeye.

Katika mantiki ya siasa za Kiafrika, ni dhahiri kwamba huyu anayeibuka kusema anataka kumwondoa mtu aliye madarakani ndiye mkorofi, kwa sababu kazi anyoitaka ina mtu tayari, na mtu huyo anaifanya vizuri tu. Haionekani sababu ya mtu mwingine kutaka kuchukua kazi ambayo tayari ina mtu na mtu anaifanya vizuri isipokuwa mkorofi tu.

Kabla hajashindwa mkorofi huyo atafanyiwa kila aina ya vituko ili kumsaidia kuelewa kwamba anachojaribu kukifanya hakiingiii akilini. Atafuatwafuatwa na mawakala wa vyombo vya dola; atasongwasongwa ili asijisikie huru na mwenye nafasi ya kutenda; atapelekewa maneno ya kumtisha na kumkatisha tamaa; atachunguzwa na asasi zinazohusika na kodi au jinai; atadodoswa kuhusu maisha yake binafsi; atachokonolewa kama vile ni nyoka na watu wanataka kuona miguu yake....

Kila juhudi zitafanywa ili kumzuia na labda kumfanya aache dhamira yake ya kutaka kuchukua kazi ambayo tayari inayo mtu na mtu huyo anaifanya vizuri. Baada ya vitisho na kila aina ya hekaheka na uchaguzi ukafanyika, huyo mkorofi akishinda wale walio madarakani wanaweza wakaukataa ushindi huo, wakaufuta. Wanaweza kufanya hivyo kwa sababu uwezo wanao, majeshi wanayo na asasi za utawala zote wanazo.

Imetokea mara kadhaa katika nchi za Kiafrika kwamba wananchi wanapiga kura kumchagua mtu fulani au chama fulani, lakini waliomo madarakani wanakataa, tena kwa nyuso kavu kabisa, kuachia madaraka.

Katika nchi kama hizo, wale waliopigiwa kura na wananchi lakini wakapokonywa ushindi ndio wanaoonekana kama wakorofi, hasa kama wananchi waliokasirishwa na udhalimu wataasi. Waliobiwa ndio wanakuwa watuhumiwa wakuu, na watuhumu wao ni wale waliowaibia.

Sitaki kusema kwamba kila mara walioshindwa wanakuwa wameibiwa, la hasha. Hutokea kwamba walioshindwa wameshindwa kweli, lakini zahama wanazozipata bado ni zile zinazoashiria kwamba ni wakorofi na wavurugaji kwa sababu tu walidiriki kutaka kuchukua nafasi isiyokuwa yao. Watapatilizwa kwa kosa hilo ambalo limeruhusiwa na katiba ya nchi.

Haya si ya kutunga, haya si ya kuzua, mifano tunayo tele. Ukweli ni kwamba Waafrika wengi bado hawajakubali msingi wa siasa za ushindani, bado. Bado tuko katika enzi za ‘mwenye nguvu mpishe’ na hapa nguvu ina maana nguvu za mabavu ya vyombo vya dola, au nguvu za mabavu mbadala, kwani wale wanaohisi wameonewa wanaweza pia kujenga uwezo wao wa kimabavu.

Kwa jinsi hii Waafrika tunajidumaza, hatuendi ko kote. Haishangazi, basi, kwamba baada ya nusu karne ya Uhuru na utawala wetu wenyewe, umasikini unazidi kukua, adha zinazidi kutuandama na ghadhabu za wananchi zinazidi kupanda. Sijui kama watawala wetu wanaliona hilo, na kama wanaliona sijui kama wanaamini kwamba njia ya kukabiliana nalo ni kutoa matamshi ya kutishana.

Matamko ya hivi karibuni kutoka kwa vyombo vilivyo karibu mno na utawala yanatia shaka kwamba watawala wanataka kuwafanya wananchi waamini kwamba wale wanaowapinga ni wakorofi na wachokozi. Inatia hofu kwamba labda na sisi hatujaondokana na mantiki niliyoieleza hapo juu. Matamko haya hayafai kwa sababu ni ya hatari.

Tunahitaji kufanya hadhari kubwa ili kuepusha janga kuu.

Wednesday 6 October 2010

Mficha uchi hazai

Mimi naitwa jina langu Sijali nimelelewa na nyanya wangu nikiwa mdogo na kwa babati nzuri nikasoma elimu chekechea katika kituo cha wazungu. Sasa raha na tabu ya umombo na mchanganyiko wa lugha za kigeni kutoka ulaya zilinisababisha kuwa na wakati mgumu sana pale gharama ya kusoma shule pamoja wazungu ilipokuwa kubwa kuliko uwezo wa kifedha kumudu gharama ya ada kutoka kwa nyanya wangu. Basi nikalazimika kujiunga na darasa la kwanza kwenye shule zetu za serikali.

Lugha rasmi katika shule za msingi hapa Tanzania kama inavyofahamika ni Kiswahili tangu darasa la kwanza mpaka kufikia darasa la saba. Ingawa kwa wakati huo lugha ya kiengereza ilitumika kama somo utakapofikia darasa tatu. Sasa hali ilikuwa ngumu kweli kwa upande wangu katika kusoma na kuandika lugha ya Kiswahili, ingawa kuongea haikuwa shida.

Somo la hisabati kwa sababu lenyewe sehemu kubwa ya shughuli zake za kiada zinategemea tarakimu na pia kama lugha moja duniani. Hivyo haikuwa na shala isipokuwa tuu. Iwapo swali kama linatakuwa limeandikwa ama kutungwa kwa maneno ya Kiswahili basi hali iliendelea kuwa mbaya.

Kimsingi nilikuwa sijishughulishi kabisa na hali hiyo maswali yanayokuwa na maelezo tena hasa ya Kiswahili, nikitegemea kwamba iwapo sitajibu basi yale maswali hisabati yenye tarakimu ambayo nilikuwa mzuri sana kwenye hilo yatanilinda kupata alama. Kitu cha kusikitisha masomo mengine yote yaliobaki yalikuwa na sifa(kusoma na kuandika,) ambazo mimi sikuwanazo.

Sasa kwa sababu za bora liende la mwalimu wetu wa darasa la kwanza, na wakati huo ilikuwa mwalimu anayeanza wanafunzi darasa la kwanza alikuwa akiendelea na wanafunzi kuingia darasa la pili. Hivyo mimi niliendela na ubovu wangu huo bila ya kupata usaidizi wa karibu wa kutoka mwalimu na mimi kama mwanafunzi nisiye fahamu kwamba hicho nachofanya kitaniletea madhara maishani.

Nikawa naona ni unafuu na ujanja kumtoroka mwalimu na kuishi kama mwanafunzi ambaye hawezi kusoma ama kuandika.Sasa hapo nyumbani nilipokuwa naishi ndipo palipoweza kugundulika udhaifu wangu maana huyo nyanya yeye kitaaluma alikuwa ni Mwalimu.

Siku moja akaniomba ripoti ya kimasomo yangu ya jumla ya mwaka ya darasa la pili wakati huo tulikuwa tunakabidhiwa wanafunzi na kuleta nyumbani . Mimi nilikuwa na ujanja wa kubadirisha tarakimu.

Hivyo nilijichanganya zile sehemu ambazo unatakiwa ujue kusoma na kuandika lugha kiswahili ili kuweza kurekebisha. Sasa sehemu inayojaza na nafasi ya mwanafunzi darasani kwenye tarakimu ilionyesha nipo nafasi ya kumi na nane kati ya wanafunzi mia moja, Ingawa ukweli wenyewe nilikuwa na nafasi ya tisini na nane.

Na hiyo ndiyo maneno yalikuwa yameandikwa kwa lguha ya Kiswahili. Basi nyanya yangu akashtukia kitu pale.Akasema naomba kachukue kile kitabu cha darasa kwanza cha Juma na Roza, Nategemea kila mtu aliyesoma wakti huo anakifahamu vizuri. Akafungua ukurasa mmoja nisome. Nilipoona tuu picha nikakumbuka ile hadithi niliyosomewa na baadhi marafiki zangu niliyokunasoma nao. Nikaaanza kusoma kwa jinsi nilivyokariri. Maana suala ilo nilikuwa mzuri na hodari sana wakukariri.

Nyanya yangu aukupata kitu hapo ingawa bado taaluma yake ilikuwa inamwambia kuwa kuna kitu kinaendelea upande, baada ya kuona mkorogo kwenye taarifa yangu ya mwaka ya kimasomo. Sasa tatizo kubwa ilikuwa wakati huo shule zimefunga hivyo hawezi kufuatilia mpaka ya mwezi na nitakuwa naingia darasa la tatu.

Kutokana na hali basi alihamua kunikabidhi kwa mwalimu mwenzake ambaye anasifikia kwa kufundisha vizuri na kufuatilia maendeleo ya mwanafunzi. Basi ya baada kufungua shule niliambiwa na Nyanya yangu kwamba nalazimika kukaa na huyo mwalimu kwenye darasa kwa muda wa juma moja kabla sijaendelea na darasa la tatu.

Kwa kuanzia tuu yule mwalimu alikuwa hatumii kitabu katika kusoma ama kuandika. Hivyo hadithi yeyote iliyopo kitabuni inaandikwa ubaoni tena bila picha. Sasa hapo na mimi nilikuwa nimepangiwa nikahe kiti cha kwanza kabisa, na pia nilichaguliwa kuwa mtu wa kwanza kusoma kwa siku hiyo, tena unatumia fimbo kuonesha maneno unayosoma, neon moja baada la jingine.

Na hapo ndiyo siri yangu ilipofichuka tena darasa lote wakijua kwamba siwezi kusoma na kuandika Kiswahili. Na pia hiyo taarifa ikawa imemfikia Nyanya wangu. Na hiyo ndiyo ilikuwa tiketi ya kubaki lile darasa la pili badala ya kuendelea darasa la tatu.

Nakubali na pia naamini yule mwalimu aliyetumia ujanja wa kujua siri yangu na nyanya wangu hawa wote walikuwa wananitakia mema maishani mwangu. Maana huyo mwalimua na huyo nyanya wote wamefariki hivi sasa wakati naandika hii habari kwa kifupi kuhusu maisha yangu huko nyuma.

Kimsingi nataka kuzungumzia siasa za hapa nyumabani Tanzania kwamba wananchi waache kuchagua viongozi kwa mazoea maana hayawezi kukusaidia kwa mikakati ya muda mrefu. Iwapo unahitaji maendeleo tusiendelee mpaka watokee malaika kama hawa walionisaidia mimi leo kuweza kujua kusoma, kuandika Kiswahili.

Kupiga kura kwa kiongozi kwa sababu mazoea utaishia kuwa kama mimi nilivyokuwa katika elimu ya awali mzuri wa tarakimu tuu na siyo maandishi anayepata hasara hapo ilikuwa ni mimi, Wakti mwalimu yeye alikuwa akiendelea kulipwa mshahara wake. pamoja kuwa nilikuwa sipati maarifa yoyote kutoka kwa yule mwalimu wa kwanza. Hivyo unapochagua viongozi wabovu pia inapelekea kuwa na maamuzi mabovu.

Siasa ni muhimili wa nchi kwa kila jambo, tusichagua wabunge, madiwani na hta pia rais kwa ajili ya mazoea. Iwapo kama tunataka na pia tunahitaji maendeleo basi hilo halina mjadala kiongozi anatakiwa awe shupavu wa utendaji anafuata misingi na sheria zilizopo na siyo maneno na ubabaishaji.

Ambayo kimsingi kama ni Rais, au mmbunge ataendelea kupokea mshahara na posho. Wakati huo huo sisi wapiga kura tukiendelea kuwa maisha shida na dhiki isiyokuwa na kipimo.

Inaendeleo siku zijazo hizi zitakuwa makala mfululizo kadri navyopata muda wa kuandika

Thursday 12 August 2010

Nakala chapishi


KATIKA hali tuliyoishuhudia wakati wa kura za maoni ndani ya chama - tawala si rahisi kwa ye yote anayefuatilia masuala ya siasa za nchi hii kupuuza masuala yaliyojitokeza. Masuala haya ni mengi, na bila shaka tutaendelea kuyajadili kwa muda mrefu, lakini wiki tunaweza kuyagusia baadhi yake kabla hayajapoa.

Kwanza, kama nilivyosema wiki jana, siasa za chama-tawala kunyata. Mambo tuliyoyashuhudia katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM yanakifu, yanachusha, yanatia kinyaa.

Lakini ni zaidi ya hayo. Kuchusha pekee, ama kutia kinyaa, si jambo jema na wala si hali ya kupendeza. Mtu anaposema anaona kinyaa, labda athari kubwa inayoweza kumtokea ni kupata kichefuchefu na hatimaye kutapika. Kwa yale tuliyoyaona mwaka huu, si uongo kusema kwamba kama kuna watu miongoni mwetu ambao bado wana chembe za uungwana, wamepata kichefuchefu, na wengine labda walijisikia kutapika.

Lakini kichefuchefu si sawa na kifo, na hutokea mtu aliyekolewa na kichefuchefu akafikia hata hatua ya kutapika na bado asife iwapo kutapika kwake hakutokani na maradhi yaliyo mwilini mwake bali ni kutokana na kichefuchefu kinachotokana na hali ya kuudhiwa na kuwa na kinyaa. Binadamu wanao uwezo mkubwa wa kushuhudia mambo ya kuudhi na bado wasife kutokana nayo.

Hata hivyo, mambo hayo yanaudhi, yanakera. Isitoshe, baadhi ya yale tuliyoyashuhudia siyo tu yanaudhi, ila pia yanatisha. Yanatishia usalama wetu kama Taifa kwa sababu yanao uwezo wa kutupeleka mahali ambako hatukutarajia kwenda, mahali pa kutuhilikisha.

Niliwahi kueleza kwamba tumeanza kutumia lugha nyepesi kuelezea dhana nzito. Nimekuwa nikijaribu kueleza kwamba kile tunachokiita ‘kero’ mara nyingi si kero bali ni janga, ni hatari, ni saratani, ni ukoma. Rushwa, kama rushwa, ndani ya jamii haiwezi kuwa kero; ni janga kwa sababu inao uwezo wa kuua jamii nzima.

Lakini, pia, rushwa ni kielelezo kimojawapo cha uoza, na vielelezo vipo vingi. Katika michakato ya uchaguzi, ni kweli, tumeshuhudia vitendo vya rushwa, kwa maana ya watu kugawa fedha na wengine kupokea fedha hizo kwa madhumuni ya kuathiri matokeo ya uchaguzi. Hiyo ni rushwa kama ile anayotoa mtu mwenye shauri mahakamani kumpa hakimu, au mtu mwenye tatizo la kiusalama kumpa askari polisi.

Uoza wa aina hiyo umetokea sana katika mchakato wa kura za maoni ndani ya chama-tawala, na ni vyema kuukemea kwa nguvu zetu zote, na ni lazima kukataa na kutupilia mbali kauli za kipuuzi za watu kama wasemaji wa chama-tawala niliowasikia. Upuuzi ukisikika, tujifunze kuutaja kama upuuzi, na huu ni upuuzi.

Sasa, ndani ya chama-tawala wametokea wahuni waliohamia huko na kisha wakapewa kibarua cha kutoa matamko ya kipuuzi mara kwa mara, maneno yenye mantiki iliyopinda na isiyoweza kumshawishi hata mgonjwa wa Mirembe. Hawa wanajulikana, asili yao inaeleweka, na kwa maana hiyo hawashangazi wanapotoa matamko yasiyokuwa na mantiki yo yote ila tu kujaza nafasi katika vyombo vya habari kwa sababu ni muhimu kwa wanajamii kujua kwamba chama-tawala kimejibu shutuma hii au ile.

Lakini kwa kuwaendekeza wapuuzi kama hawa, na kuwazoea kama wasemaji wa mara kwa mara wa chama-tawala, ipo hatari kwamba hata watu wasiotarajiwa kutamka maneno ya kihuni kuingia katika mkumbo huo na kujisemea tu, alimradi wamesema. Mazoea huzaa hulka, na hulka huzaa utamaduni.

Ndivyo ninavyomwangalia Pius Msekwa, makamu mwenyekiti wa chama-tawala, na jinsi anavyozungumzia janga kubwa la uoza ndani ya chama chake. Msekwa anasema kwamba, na anataka tuamini kwamba tatizo la rushwa haliwezi kuwekwa mlangoni kwa chama chake, kwa sababu ni tatizo la Taifa zima.

Hapa kama kuna mtu amemwelea Msekwa, naomba anisaidie. Ni kweli tatizo la rushwa ni la Taifa zima, lakini kwa nini liseelekezwe kwa chama-tawala, chama ambacho, kama wanavyotamba wasemaji wake, ndicho kilichopewa dhamana ya kuongoza Taifa letu? Ni chama hicho kilichoomba, tena kwa nguvu za fedha na jeuri za aina nyingine, kipewe madaraka ya kuongoza nchi yetu, na hiyo dhamama kikapewa.

Sasa, kama nchi nzima imejaa rushwa, kama alivyoeleza Msekwa kwa ufasaha mkubwa, sisi tumwulize nani kama si chama hicho? Lakini labda Msekwa, kwa kuathirika kutokana na ule upuuzi ulioingizwa ndani ya chama chake na wale wahuni niliowataja mapema, alisahau kwamba alikuwa anaulizwa swali kuhusu chama chake.

Ni kweli, kama anavyosema Msekwa, rushwa iko polisi, iko mahakamani, iko hospitalini, iko vyuoni, iko kila mahali. Lakini ukweli huo hauwezi kuwafanya wadadisi wasimuulize Mkuu wa Polisi kuhusu rushwa katika jeshi lake, au wasimuulize Jaji Mkuu kuhusu rushwa katika mahakama zake, na kadhalika. Sijui Msekwa alitaka nani aulizwe kuhusu rushwa ya kutia kinyaa katika mchakato wa kura za maoni ndani ya chama chake. Tumwulize Waziri wa Afya?

Watu kama Msekwa wanatakiwa waache upuuzi kwani dhamana waliyo nayo ni kubwa mno, wakiendelea na upuuzi wao sote tutaathirika. Hii ndiyo sababu sichelei kumwambia Msekwa kwamba umri wake, uzoefu wake, historia yake, elimu yake na hadhi yake.. vyote hivi havimpi ruksa ya kuzungumza kihuni. Chama chake kimewapa ajira wahuni wengi ambao wanatosha kabisa kutuchekesha huku tukilia machozi.

Hata hivyo, najua kwamba uhuni huu ukiachiwa ukaendelea, siku moja hata hicho kicheko katikati ya machozi kitakatika, na kilio kitakuwa ni cha moja kwa moja. Msekwa anataka kutuambia kwamba hata udanganyifu wa viongozi na watumishi wa chama chake si tatizo la chama chake?

Kama Msekwa na wakuu wengine wa chama-tawala hawaoni kwamba uingizaji wa kadi bandia za uanachama katika michakato ya ndani ya chama hicho si tatizo la chama, ni nini wanachokiona? Hujuma kama hii ingefanywa na chama kingine kinachotaka kukidhoofisha chama-tawala, ingeeleweka. Kwamba watu ndani ya chama hicho wanakihujumu kwa makusudi kabisa halafu wakubwa wake hawaoni kwamba kuna tatizo, ni uthibitisho kamili kwamba nchi hii imo mikononi mwa watu wa kutisha.

Kumbukumbu zangu zinaniarifu kwamba mwaka 1977, katikati ya sherehe zilizotangulia muungano wa TANU na ASP kuunda CCM, Pius Msekwa alikuwa Katibu Mtendaji Mkuu wa CCM. Katika hafla mojawapo ya maadhimisho hayo, Msekwa alitoa tamko lililosema kwamba jina ‘Chama Cha Mapinduzi’ halikuwa na maana kwamba kila mwanachama wake angetakiwa kuwa mwanamapinduzi.

Hii bila shaka ilikuwa na maana kwamba mtu hakuhitaji kuamini itikadi yo yote ili kuwa mwananchama wa CCM. Lakini aliyekuwa rais wa ASP, Aboud Jumbe, alimkosoa Msekwa kwa kubainisha kwamba ili kuwa mwanachama wa chama kinachoitwa cha mapinduzi ni mantiki ya kawaida kwamba lazima mtu awe mwanamapinduzi. Leo nadhani kwamba mshindi katika ubishi huo wa miaka thelathini na tatu iliyopita ni Msekwa. Naamini ndiyo maana bado anakiongoza chama chake cha mapinduzi kisichokuwa na wanamapinduzi.

Hata kama tutakubali kwamba sisi sote tu vipofu, si tumsikilize Bwana Issa bin Maryam, aliyetufundisha kwa kuuliza swali hili: Je, kipofu anaweza kumwomgoza kipofu mwenziwe? Si wote watatumbukia katika shimo?

Itaendeelea.

Wednesday 2 June 2010

The curious case of Samuel Eto'oJune 2, 2010

Email Print By Tom Adams
(Archive)
The 2010 World Cup, coming to Africa for the first time, was supposed to showcase the best of the continent, but recent weeks have generated cause for concern. Ghana have lost Michael Essien to injury, both they and Cameroon suffered heavy defeats to European opposition on Tuesday night and Ivory Coast installed a brand new coach so close to the tournament. But the most worrying problem appears to surround Samuel Eto'o, perhaps the leading African player of his generation.


GettyImages
Samuel Eto'o has plenty to ponder at present
Over the weekend, Eto'o threatened to quit the national side and forego the chance to appear in his third World Cup finals after being stung by criticism from Roger Milla, Cameroon's hero of 1990 as they unexpectedly reached the quarter-finals. Milla accused Eto'o of failing to replicate his club form at international level, leading to a passionate response.

"People should respect me and they must shut up, really shut up, because playing in the World Cup quarter-finals is not the same as winning the World Cup," Eto'o said. "It is always before tournaments that bitter people wake up. What has he [Milla] done? He hasn't won the World Cup... And then you wonder, 'are they my people?' Are they really my people?' Is it worth me going to the World Cup? I've still got some days to think about it but I'll see if my taking part is important because I don't need this in my career."

He was subsequently included in Paul Le Guen's 23-man squad for the finals but on Tuesday his body language was instructive as he was sent off in a 3-1 friendly defeat to Portugal. Eto'o received a second yellow card for a high tackle on Duda and gesticulated furiously to the referee as well as becoming involved in an argument with Cristiano Ronaldo. Le Guen attempted to calm him down but it appears that the striker, who has won back-to-back Trebles with Barcelona and Inter Milan, is far from happy in an international shirt at present.

What impact this has on Cameroon's challenge remains to be seen, but ahead of a tournament in which the continent of Africa hoped to shine, the cloud around Eto'o is another worrying sign.

O BROTHER, WHERE ART THOU?

Players of all nationalities were left bitterly disappointed this week when all 32 countries had to submit their final 23-man squads to FIFA, but the exclusion of Mexico's Jonathan Dos Santos provoked perhaps the most extreme reaction. The 20-year-old - who has started just three games for his country, two more than at Barcelona - was no doubt disappointed to discover he would not be joining older brother Giovani in Javier Aguirre's selection, but his father was furious. Zizinho, a former professional himself, has claimed Jonathan will no longer represent the country and that Brazil and Spain could be viable alternatives. Giovani's participation is also in doubt.

"Gio is very hurt and he wants to be at home with us," said Zizinho. "He is there now and he's not well. We don't know if he will play (at the World Cup) or not. We still don't know anything. Jonathan told me that he is going to quit the Mexican team and I don't want him playing for them anymore anyway." While the Dos Santos family are no doubt disappointed by Monday's news, ending Giovani's international career as well would seem bizarre, and more than a little petulant.

PLAYER IN FOCUS: Fabio Quagliarella


GettyImages
Fabio Quagliarella edged out Giuseppe Rossi and Marco Borriello
The Napoli forward was the surprise inclusion in Marcello Lippi's 23-man Italy squad announced on Tuesday as he was included at the expense of the up-and-coming Giuseppe Rossi. Quagliarella scored just 11 goals in Serie A this season, some eight less than Palermo's Fabricio Miccoli who was not even considered in the Azzurri's preliminary squad. Emile Heskey will, perhaps unconvincingly, tell you it is not all about goals at international level, and Quagliarella's versatility appears to have won him a place on the plane to

Monday 31 May 2010

Kakobe: ufisadi hauwezi kuisha chini ya uongozi wa kifisadi


Elizabeth Ernest

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Felloship (FGBF), Zachary Kakobe amesema ufisadi nchini hauwezi kumalizika iwapo nchi itaendelea kuongozwa na mafisadi.

Akihubiri katika Ibada kwenye kanisa hilo lilliloko Mwenge jijini Dar es Salaam juzi Jumapili, Kakobe aliwataka waumini wake kujiunga katika vyama vya siasa na kugombea nafasi za uongozi ili waiongoze nchi.

Alisema kwa sasa nchi inatawaliwa na mafisadi na ndio sababu wamejenga dhana ya “chukua chako mapema” kwa kukosa hofu ndani ya mioyo yao kwa uovu wanaowatendea wanyonge.

“Wote wanaoimba wimbo wa ufisadi ni wanafiki wakubwa, tena ndio mafisadi wenyewe. Mwenyehaki akitawala baraka za Mungu zinakuja na nchi inastawi”, alisema Kakobe.


Kakobe alisema wenyehaki wakijitosa katika siasa kwa nguvu zote wataushinda ufisadi, lakini, wakikaa pembeni, ufisadi hautakwisha na kwamba nchi itaendelea kutawaliwa katika misingi ya kifisadi.

“Mwenye haki ndiye anapaswa kuongoza, kwa sababu atasimamia haki za wanyonge, tofauti na sasa nchi inavyoongozwa ambapo kuna watu zaidi ya milioni nane hawajui watakula nini, kwa sababu nchi haiongozwi katika misingi ya sheria ya Mungu”, alisema.

Askofu huyo alisema viongozi wanaoongoza nchi hawana hekima kwa sababu hawaongozwi na Neno la Mungu, tofauti na alivyokuwa hayati Julius Nyerere aliyesema alikuwa akitembea na Biblia kila alipokwenda iliyompatia hekima katika utawala wake.

“Aliye mkamilifu anayo hekima ndani yake, nahitaji watu wenye haki wajiunge na siasa ili ufisadi uondoke kabisa katika nchi hii na wanyonge wapate haki zao”, alisema Kakobe.

Kakobe aliwataka waumini wake kujinga katika vyama mbalimbali vya siasa akieleza kuwa, hata Yesu alikuwa upande wa wapinzani na kwamba msemo wa ‘fikra kwa mwenyekiti zidumu’ sasa haupo tena.

“Jiunge na chama tawala, hata CCJ ingia nitakutia mafuta. Watu wanaosema siasa ni mchezo mchafu, wachafu ni wao wenyewe, tangu sasa dhamiria kuingia kwenye siasa”, kiongozi huyo alisema.

Kakobe alisema yeyote mwenye haki atapata ujasiri kama simba katika kupambana na mafisadi na kwamba hata yeye anao ujasiri aliosema amepata kutoka kwa Mungu.

Kiongozi huyo alliyewahi kumpigia debe Augustino Mrema wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), katika uchaguzi wa rais mwaka 2005, alisema lazima wenye haki wasimame kutumikia ufalme wa Mungu na kwa kupigana na ufisadi kwa kujitosa kwenye siasa.

Kakobe aliyewahi kulumbana na serikali katika mambo kadhaa, alisema viongozi wanaoongoza bila kuwa na hofu mioyoni mwao wanatawaliwa na nguvu za giza.

Alisema kwamba miungu ya viongozi ni tofauti na wenye haki wanaoongoza kwa sheria na misingi ya Mungu.

"Wanaoongoza bila hofu ya Mungu, muingu yao iko Bagamoyo, Sumbawanga na Pemba, tofauti na wenye haki ambao wataongoza na sheria inayotengenezwa na misingi ya Mungu",alisema.

Alisema shetani daima anataka watu wanaofanya matambiko na kwenda kwa waganga waongoze nchi, ili waendelee kufanya maisha ya wanyonge yaendelee kuwa magumu na wasijue watakula nini", alisema Kakobe.

Hata hivyo, alisema kuwa wapo watawala wanaotafsiri vibaya Neno la Mungu wakidhania kwamba mtu mcha Mungu hatakiwi kutawala, bali kutawaliwa na kueleza kuwa dhana hiyo ni uongo na potofu akisema, biblia haitafsiriwi jinsi mtu aonavyo.

Habari hii kwa hisani ya gazeti la mwananchi-Tanzania

JK hupo wapi!!!?







Breaking NewsWorld Condemns Deadly Israeli Ship Attack
Cameron: No more 'cloak of secrecy'



Buzz Up! Print StoryDavid Cameron has pledged to remove the "cloak of secrecy" from government as ministers seek to reassure the markets that the departure of David Laws will not derail plans to tackle the deficit. Skip related content
Related photos / videos
Cameron: No more 'cloak of secrecy'
Enlarge photo .Related content
Cameron To Remove 'Cloak Of Secrecy'
PM vows more openness in government
Coalition hit by minister's expense claims
Related Hot Topic: David Cameron
Have your say: David Cameron
The Prime Minister is promising the public greater access to information including hospital superbug figures, street-by-street crime data, and itemised lists of Whitehall spending.

But he also faces the continuing fallout from the weekend resignation of Mr Laws, the highly-rated Chief Secretary to the Treasury who was seen as having made a successful start to the government's cost-cutting drive.

Already, there are fresh claims in the Daily Telegraph that Mr Laws' successor, Danny Alexander, had dodged capital gains when selling a property he designated to Parliament as his second home.

Aides to the Lib Dem MP insisted he had never "flipped" designations and simply followed tax rules, meaning people are not eligible for CGT if they own two homes, but sell one within three years.

Mr Alexander, a former PR chief for Cairngorms National Park Authority, is said to have owned the south London flat for six years before becoming an MP in 2005, when he told the parliamentary authorities it was his second home. At around the same time he purchased a constituency home in Scotland. According to the Telegraph, he claimed more than £37,000 in expenses on the flat before selling in June 2007....

News for the courtsey of the sun news papers online-UK

Hawa ndiyo wapiga kura wenu CCM!!!?



Miaka nenda rudi tunaishi kwa matumaini ambayo hayapo. Je waziri Kapuya unasema nini kuhusiana muda mfanyakazi kazi kibaru unakoma baada ya muda gani ili kupata mkataba. Hawa wapiga kura wenu ninyi chama tawala wapo utumwani katika nchi yao. Ajira zao zinaanza asubuhi na kukoma jioni tena kwa muda usiokuwa na kikomo. Kifupi ajira inaanza asubuhi lakini haifahamiki muda wa kumaliza kazi.

Na hata hiyo asubuhi itategemea na saa ya utakayofika hapao kazini. Iwapo umechelewa basi nafasi siku hiyo nayo imetoweka. unatakiwa kujibidisha kufika kazini mapema ikiwezekana masaa mawili kabla kuanza kazi. Je CCM mpo hapo...kumbukeni mpo madarakani muda wa miaka thelasini na tatu kwa jina la CCM na kabla ya hapo kwa jina TANU.

Nini kipya mtakachotueleza safari hii

Ukivulia Nguo maji ni sharti kuoga mwili mzima




Iwapo tumekubali kuingia katika mfumo wa vyama vingi basi tukubali kutekeleza kila kitu na tuache visingizio ambavyo haviendani na mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Tukumbuke kuwa tulikuwa na mashirka ya umma tena mengine yalikuwa yakiendeshwa kwa ufanisi lakini tukasema serikali kazi yake ni kusanya kodi na siyo kufanya biashara na viongozi wetu wakahamua kuyauza mashrika yote, na mengine kufa kifo cha mende na pia kuuzwa kwa bei ya bure kama NBC.

Sasa tumeingie kwenye mfumo wa vyama vingi basi moja kwa moja tukubali kila kitu katika mfumo...kama hili suala la mgombea binafsi. Kwa sababu tukumbuke jamii yeytu sasa hivi inatakiwa kumshirikisha kila mpiga kura wetu ashiriki katika chaguzi mbalimbali, na siyo kila mpiga kura ni shabiki wa vyama vya siasa. Kuna wapiga kura ambao wangependa kupiga kura kwa mgombea binafsi. Na kwasababu hiyo basi mara nyingi wanashindwa kuitumia haki yao kupiga kwa kukosa mgombea binafsi....Inaendelea

Liyumba Amefungwa Jela au Walalahoi wamefumbwa Akili!!!?


Nikitafakari kwa kina naona ni wengi wapo kama Bwana Liyumba katika hizi tuhuma lakini bado sheria haijachukua mkondo wake. Kuna suala la rada hapa la ufisadi wa rada hapa na mabilioni ya EPA yaliyoingia mifukoni kwa mimi nawaita watu wenye akili kuliko sisi sote watanzania. Maana wametenda uhalifu lakini ndiyo kwanza wanaishi kama peponi na sheria na vyombo vyote vya dola vipo vikiwatazama...

Mimi Mcharikaji kuganga njaa na elimu yangu duni siwezi kupambana nao. Je na hao viongozi tuliowapigia kura wanawakilisha hao waahailfu maarufu siku hizi MAFISADI au wanatuwakilisha sisi!!?. Je kuhukumia kifungo kwa Bwana Liyumba ni kwa ajili ya kuturidhisha sisi walalahoi kuwa serikali inafanya juhudi ya kufuata utawala wa sheria. Uchaguzi mkuu bado miezi takribani mitano mpaka kufanyika au hii hukumu inaendana na mahitaji yetu au mahitaji ya hao watawala kupigiwa kura halafu turudi kama kawaida mahakamani kukata rufaa, Bado inaendelea.........

Sunday 30 May 2010

Laws quits over expenses scandalBy STAFF REPORTER

Published: 29 May 2010
Add a comment (41)
DAVID Laws has quit as Treasury chief after it emerged he channelled thousands in Commons expenses to his secret gay lover.
Lib Dem Scottish secretary Danny Alexander will take over from him, Downing Street announced last night.





Mr Laws's resignation comes as the first major blow to the Tory-Lib Dem coalition.

In a statement, Mr Laws said: "I do not see how I can carry out my crucial work on the budget and spending review while I have to deal with the private and public implications of recent revelations."

Prime Minister David Cameron described Mr Laws as "an honourable man", telling him: "I hope that, in time, you will be able to serve again."



Supportive ... PM David Cameron and deputy Nick Clegg
This morning, deputy PM Nick Clegg said he had "enormous respect" for his colleague's "dignity and integrity".

He said: "My admiration for him has only grown as I have seen how he has dealt with the cruel pressures of the last 24 hours.

"There are clearly questions that David himself acknowledges must now be answered about his own expenses.

"When these questions have been addressed, I very much hope that there will be an opportunity for him to rejoin the Government."

Mr Laws's resignation came after it was revealed he had paid £40,000 of taxpayers' money to Jamie Lundy, the man he had been dating since 2001.


There are clearly questions that must now be answered about David's expensesDeputy PM Nick Clegg

The couple had kept their relationship secret from everyone, including family and friends.

Work and pensions secretary Iain Duncan Smith today said Mr Laws was a "thoroughly decent person".

But he added: "I think on balance he is right. If you have got the toughest job in Government to try and find the savings, you cannot be beset by personal problems."

In his resignation letter, Mr Laws wrote: "The last 24 hours have been very difficult and distressing for me.

"I have been thinking carefully about what action I should take in the interests of the Government, my constituents and — most important of all — those whom I love.

Advertisement

Responding to the letter, Mr Cameron wrote: "The last 24 hours must have been extraordinarily difficult and painful for you.

"You are a good and honourable man. I am sure that, throughout, you have been motivated by wanting to protect your privacy rather than anything else.

"Your decision to resign from the Government demonstrates the importance you attach to your integrity.

"In your short time at the Treasury, you have made a real difference, setting the Government on the right path to tackle the deficit which poses such a risk to our economy."



Read more: http://www.thesun.co.uk/sol/homepage/news/2992831/Laws-quits-over-expenses-scandal.html#ixzz0pQR2S9AC

Was it a trip for tourists or Diaspora filling up in the Cupboard!!?


These are wonders of Tanzania slogans to manipulate many or few people into politics or economy or social events within Tanzania Population living abroad. Was it a trip for holiday makers!!!!

Soka ya Tanzania itabadilika kwa kucheza na Timu ya Taifa-Brazil ndani dakika tisini!?


Mtazamo wangu hupo tofauti kabisa na chanzo halisi ya matatizo ya soka ya Tanzania...Tukumbuke kuwa Brazil kiuchumi wapo juu yetu kidogo ingawa kimsingi ni wenzetu katika masuala ya mambo ya uchumi. Je wamewezaje kuweza kuwa na mafanikio ya katika soka kuliko sisi! Imekuja timu ya Taifa ya Ivory Coast imetusaidia nini? Je ni kweli baadhi ya wachezaji wetu walionekana katika runinga ya SKY na jingine zenye majina makubwa. Hivi ni kweli tunachohitaji ni kucheza na timu kubwa za Taifa!?

Kimsingi hizo pesa zilizolipwa kwa Brazili ili kucheza na timu ya Taifa ya Tanzania zingeweza kuwapeleka kusoma soka wachezaji wastaafu ya timu ya Tanzania kozi za muda mrefu na pia marefa wale wote wenye nia ya kufanya hivyo huko Brazil. Mimi nachoona tunachokosa hapo ni wataalamu wa kuendeleza vipaji, viwanja vya soka safi na salama, marefu wenye mafunzo tangu wakiwa wadogo na vifaa vya michezo. Sina sababu ya kuzungumzia viongozi wa vyama vya michezo kwa sababu hayo yatajitengeneza yenyewe iwapo tukiweza kuwa wataalamu wa soka wenye ujuzi wa kisasa.

Hivi sasa vipaji vya soka Tanzania vinajivumbua vyenyewe bila ya usimamizi wa kiutaalmu matokeo yake. Maumbile ya wachezaji wetu wengi hayaendani na nafasi wanazocheza uwanjani. Imefikiwa wakati viongozi wa soka na mashabiki huwa wanakimbilia kuwalaumu wachezaji kwamba wameongwa baada ya mechi kuwa wamecheza chini ya kiwango bila kuangalia na hao wachezaji kujitambua nafasi wanazhocheza haziendani na wao walivyo kiumbo na urefu pia....

Uzoefu wa mechi za majaribio ni kujifunza, tulipocheza na Misri na Ivory Coast nini tulichojifunza hapo!? Cha zaidi kilichotokea ni aibu tuu kufungwa magoli matano Misri. Hamasa ya wachezaji haitapatikana kwa kucheza na timu kubwa kama hii ya Brazil. Hii naweza kufananisha Mtoto anayetambaa akaharakishwa kukimbia kabla hata miguu ya huyo mtoto kutengemaa kuweza kuimilia uzito wake binafsi. na hata hao wanaosema Tanzania kwa kucheza na Brazil basi itakuwa imefahamika katika ramani ya soka ya dunia. Mimi nategemea kufahamika kwetu katika ulimwengu soka ni kwa kufungwa magoli ya aibu katika ulimwengu wa soka.

Soka yetu ina matatizo makubwa sana yanayotokana na utaalamu zaidi kuliko tunavyofikria. Leo hii nchi kama Ghana, Cameroon, Nigeria, Senegal na Ivory Coast. Wamewezaje kufikia hapo walipo. Nilitegemea hili ndiyo vitu TFF na wadau wengine wa soka wangejadili kwa kina ili kupata jibu la kudumu. Soka ni sayansi na sisi tupo nyuma sana kitaaluma. Hata hawa wataalamu tuliyonao hivi sasa wamesomea hiyo elimu wengine hata kabla ya mobile phone Technology kufika Tanzania.

Kimsingi sisi ni watawala wazuri kwa mambo ya muda mfupi kuliko mikakati ya endelevu ya muda mrefu. Tungetafakari vizuri hicho kiwango cha pesa kinachotumika kuileta Brazil ingeweza kuleta mageuzi ya kweli katika soka kwa kuwapeleka wachezaji wastaafu waliwahi kucheza timu ya Taifa na vijana ili waweze kusoma kozi ya soka za kisasa kwa nchi kama hiyo Brazil. Hayo maarifa wangeweza kwenda sasa kushirikia kikamilifu kuvumbua vipaji na maarifa watakayokuwa mwamejinza. Hivi Leo hatuna wachezi warefu katika soka na ukweli unafahamika unapokuwa mrefu kuna sifa kama mchezaji.

Maumbile ya wachezaji hayawezi kujitambua yenyewe ni sharti kuwe wataalamu wa hiyo nyanja walisomea elimu kisasa ndiyo waweze kufmumbua. Makocha wa kigeni ni muhimu kuwa kwa timu ya Taifa lakini suala kubwa ni lilelile. Kocha mzuri wachezaji siyo wazuri kwa sababu mchezaji wa timu ya Taifa anapoitwa timu ya taifa ni vyema kwa huyo mchezaji kuwa tayari kisoka lakini siyo hawa tulikuwa nao. Wengi wao bado wanahitajika tena kufundishwa hata jinsi ya kufnga goli. na hiyo siyo sifa mchezaji anayeitwa kuja kuchezea timu ya Taifa. Kocha wa Timu Taifa anakuja kutengeneza patern ya uchezaji siyo kukufundihsa jinsi ya kumiliki mpira.

Iwapo mtu yeyote angependa kushiriki huu mjadala anakaribishwa....

Friday 28 May 2010

Tanzania tunaelekea kwenda mbele au tunarudi walipokuwa mababu zetu!!!!???


Mpaka karne hii ya ishirini na moja tunatumia usafiri huu..Je safari ya kufikia maendeleo ya kweli ipo!!!!!!!!???????

Saturday 22 May 2010

Chanzo cha Ajali za barabarani Tanzania nini!


Imekuwa kawaida kwa jamii na serikali kuwatupia lawama Madereva, wamiliki wa magari kuwa ndiyo wanasababisha ajali na kwa sababu ya uzembe wa madereva!!!!!!!!. Je hiyo kweli ni sababu ya kweli ama kuna sababu zaidi ya hizo..
Picha kwa hisani ya Michuzi Blog